Tuesday, February 28, 2017

RAIS WA FIFA AKANUSHA KUWA NA MIPANGO YA KUMNG'OA HAYATOU.

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Gianni Infantino alikuwa nchini Ghana jana na kupuuza madai kuwa anashawishi rais wa Shirikisho la Soka la Afrika-CAF Issa asiungwe mkono katika uchaguzi wa shirikisho hilo. Infantino alikuwa katika taifa hilo kutoka madharibi mwa Afrika ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya bara hili ambapo pia imeshuhudia akipita katika nchi za Afrika Kusini, Zimbabwe na Uganda. Akiwa nchini Zimbabwe, Infantino alihudhuria sherehe ya siku ya kuzaliwa ya rais wa Shirikisho la Soka la nchi hiyo Philip Chiyangwa hatua ambayo ilizua maswali mengi. Chiyangwa ambaye ni mfanyabiashara pia alitumia mwanya huo kusherekea kuchaguliwa kwake kuongoza Baraza la Michezo la nchi za Kusini mwa Afrika-COSAFA na kuwaalika viongozi kadhaa wa soka ambao hawamuungi mkono Hayatou. Hayatou ambaye anatarajiwa kugombea kipindi kingine cha nane katika uchaguzi utakaofanyika Machi mwaka huu, anatarajiwa kupata upinzani kutoka kwa rais wa Shirikisho la Soka la Madagascar Ahmad Ahmad ambaye meneja kampeni wake ni Chiyangwa.

No comments:

Post a Comment