Tuesday, February 28, 2017

ZAMPARINI KUJIUZULU PALERMO.

RAIS wa Palermo, Maurizio Zamparini anatarajiwa kujiuzulu wadhifa wake huo ka klabu hiyo ya Serie A baada ya kuiongoza kwa miaka 15. Taarifa zimedai kuwa Palermo inatarajia kutangaza mbadala wake ndani ya siku 15 zijazo kufuatia timu hiyo kupata mmiliki mwingine. Katika kipindi cha miaka 15 ya Zamparini imeshuhudia makocha kadhaa wakija na kuondoka katika klabu hiyo wakiwemo 10 katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita. Zamparini aliinunua Palermo wakati ikiwa inashiriki Serie B mwaka 2002 na kuingoza kupanda katika Serie A msimu wa 2003 na 2004. Hata hivyo, Zamparini mwenye umri wa miaka 75 anaiacha Palermo ikiwa inashikilia nafasi ya 18 katika msimamo wa ligi hiyo huku wakiwa alama saba nje ya eneo la kutoshuka daraja baada ya kucheza mechi 26.

No comments:

Post a Comment