Tuesday, February 28, 2017

MENEJA WA MUDA WA LEICESTER AJINADI BAADA YA KUSHINDA.

MENEJA wa muda wa Leicester City, Graig Shakespeare amesema yuko tayari kupewa kibarua cha kudumu baada ya kuiongoza klabu hiyo kuichapa Liverpool mabao 3-1 kwenye mchezo wake wa kwanza. Shakespeare alipewa nafasi hiyo kutoka ile ya usaidizi aliyokuwa nayo awali kufuatia kutimuliwa kwa Claudio Ranieri Alhamisi iliyopita, miezi tisa baada ya kuwasaidia kubeba taji la Ligi Kuu. Akizungumza na wanahabari waliomuuliza kuhusiana suala hilo, Shakespeare amesema anadhani yuko tayari kwa majukumu ya kudumu kuinoa klabu hiyo lakini anawaachia wamiliki waamue. Mabao mawili ya Jamie Vardy na moja ya Danny Drinkwater yalitosha kuwapata Leicester ushindi huo na kufufua matumaini yao kupigana kutoshuka daraja, huku bao la Liverpool likifungwa na kiungo Philippe Coutinho.

No comments:

Post a Comment