Tuesday, February 28, 2017

KLOPP AKIRI KIBARUA KUWA MASHAKANI.

MENEJA wa Liverpool, Jurgen Klopp amekiri kuwa mustakabali wake uko mashakani kama akishindwa kuinua kiwango cha wachezaji wake kilichoshuka katika mechi za karibuni kufuatia kipigo kizito kutoka kwa Leicester City jana. Kipigo hicho kinakuwa cha tano kwa Liverpool katika mashindano yote msimu huu, na ingawa klabu hiyo ndio pekee ambayo haijafungwa na wapinzani wanaoshikilia nafasi sita za juu, Klopp anafahamu yeye pamoja na wachezaji wake wanacheza na mustakabali wao. Akizungumza na wanahabari Klopp amesema wamekuwa wakifuatiliwa kila siku yeye pamoja na wachezaji hivyo wasipobadilika na kurejesha makali yao ni wazi mustakabali wao utakuwa mashakani. Liverpool imefungwa mechi nne ugenini msimu huu dhidi ya Burnley, Bournemouth, Hull City na Leicester wakati pia wamepoteza mechi moja ya ugenini dhidi ya Swansea City na kuwaacha katika hatari ya kushindwa kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment