Tuesday, February 28, 2017

RIBERY FITI KUIVAA SCHALKE KESHO.

MENEJA wa Bayern Munich, Carlo Ancelotti amethibitisha kuwa Franck Ribery yuko fiti kwa ajili ya kuivaa Schalke 04 kesho huku kukiwa na wasiwasi wa Renato Sanches na David Alaba kukosa. Ribery hajacheza mechi yeyote toka ile waliyoshinda mabao 2-1 dhidi ya Werder Bremen Januari 28 kufuatia kupata majeruhi ya msuli, lakini alikuwepo benchi la wachezaji wa akiba wakati Bayern ilipoibugiza Hamburg mabao 8-0 Jumamosi iliyopita. Bayern wanakabiliwa na ratiba ngumu katika wiki ya kwanza ya Machi, kwnai mchezo wao war obo fainali ya DFB-Pokal itafuatiwa na safari ya mchezo wa Bundesliga dhidi ya Cologne na ule wa hatua ya timu 16 bora ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Arsenal. Mechi zote hizo za Bayern zitachezwa ndani kipindi cha siku saba. Akieleza mikakati yake, Ancelotti amesema anadhani atakuwa tayari kumpumzisha Douglas Costa na kumpa nafasi Franck Ribery kwasababu tayari yuko fiti. Hata hivyo meneja huyo aliendelea kudai kuwa bado hana uhakika na Alaba aliyepata majeruhi madogo pamoja na Sanches aliyekuwa akisumbuliwa na maradhi.

No comments:

Post a Comment