Tuesday, February 28, 2017

JEROME VALCKE APINGA KUFUNGIWA MIAKA 10.

KATIBU mkuu wa zamani wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Jerome Valcke amekata rufani kupinga adhabu ya kufungiwa miaka 10 kujishughulisha na masuala ya soka. Valcke aliyekuwa msaidizi wa karibu wa rais wa zamani wa FIFA Sepp Blatter, alifungiwa mwaka jana kwa tuhuma za kujihusisha na sakata la kujipatia fedha kwa kulangua tiketi za Kombe la Dunia. Valcke raia wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 56, sasa amekata rufani Mahakama ya Kimataifa ya Michezo-CAS kupinga adhabu hiyo. Mara zote Valcke amekuwa akikanusha kufanya jambo lolote kinyume cha sheria. Awali alikuwa amelimwa adhabu ya kufungiwa miaka 12 na faini ya paundi 70,800 na FIFA, ingawa baadae adhabu hiyo ilipunguzwa.

No comments:

Post a Comment