Tuesday, February 28, 2017

RAIS WA UEFA AIONYA MAREKANI.

RAIS wa Shirikisho la Soka la Ulaya-UEFA, Aleksander Ceferin amesema kuwa kama Marekani itweka sheria za kuzuia wageni kuingia nchini humo inaweza kuathiri maombi yao kutaka kuwa wenyeji wa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2026. Rais wa Marekani, Donald Trump yuko katika mchakato wa kujaribu kufungia wahamiaji kutoka nchi saba za kiislamu kutoingia nchini humo, kufuatia mahakama kuu kusimaisha zoezi hilo mara ya kwanza. Ceferin ana wasiwasi kuwa hatua kama hiyo inaweza kuwaathiri wao wenyewe katika mbio zao za kujaribu kuwa wenyeji wa Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza toka mwaka 1994. Akizungumza na wanhabari, Ceferin amesema hatua hiyo ya Marekani ana uhakika haitawasaidia kupata nafasi ya kuandaa Kombe la Dunia kwasababu kama wachezaji hawataweza kwenda kwa ajili ya uamuzi wa kisiasa au vinginevyo ni wazi michuano hiyo haitaweza kuchezwa eneo hilo

No comments:

Post a Comment