Friday, February 24, 2017

SIMBA NA YANGA HAPATOSHI TAIFA.

LIGI KUU Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea tena leo kwa mchezo mmoja utakaowakutanisha mahasimu timu za Simba na Yanga. Mchezo huo ambao unaotarajiwa kushuhudiwa na maelfu ya mashabiki kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi utafanyika katika Uwanja wa Taifa wa Dar es Salaam baadae leo. Simba watakaokuwa wenyeji wa mchezo huo wataingia uwanjani wakiwa vinara wa ligi wakipishana na wapinzani wao Yanga wenye mchezo mmoja mkononi kwa tofauti ya alama moja. Simba waliokuwa wameweka kambi yao ya maandalizi huko Pemba wametua jijini mapema jana huku wakijinasibu kuibuka na ushindi katika mchezo huo wakati wapinzani wao waliokuwa wameweka kambi yao nje kidogo ya mji huko Kimbiji nao wakitoa majigambo yanayofanana. Mwamuzi katika mchezo huo anatarajiwa kuwa Methew Akram kutoka Mwanza atakayesaidiwa na Mohammed Mkono wa Tanga na Hassan Zani wa Arusha watakaoshika vibendera. Uhuru FM itawatangazia pambano hili la watani wa jadi moja kwa moja kutoka Uwanja wa Taifa hivyo usikose kusikiliza.

No comments:

Post a Comment