Friday, February 24, 2017

MKHITARYAN KUIKOSA FAINALI YA EFL.

MENEJA wa Manchester United, Jose Mourinho amethibitisha kuwa Henrikh Mkhitaryan hatarajiwi kuwa fiti kwa ajili ya mchezo wao wa fainali ya Kombe la EFL dhidi ya Southampton kesho. Hata hivyo, nahodha Rooney anatarajiwa kuwepo katika kikosi hicho kufuatia nyota huyo kutoa taarifa kuwa anataka kuendelea kuitumikia United Alhamisi iliyopita. Akizungumza na wanahabari, Mourinho amesema kiungo Michael Carrick atakuwepo katika kikosi chake lakini Mkhitaryan hatakuwepo baada ya kupata majeruhi katika mchezo wa Europa League dhidi ya Saint-Etienne Jumatano iliyopita. United watavaana na Southampton wakati wakiwania kupata taji lao pili msimu huu baada ya kutwaa Ngao ya Hisani mwanzoni mwa msimu.

No comments:

Post a Comment