Friday, February 24, 2017

ROONEY AKANUSHA TETESI ZA KUTAKA KWENDA CHINA.

MSHAMBULIAJI wa Manchester United, Wayne Rooney amepuuza taarifa za mazungumzo ya kwenda China na kudai kuwa bado ataendelea kubakia Old Trafford. Rooney mwenye umri wa miaka 31, amekuwa akihusishwa na tetesi za kwenda Ligi Kuu ya China ambapo dirisha lao la usajili linafungwa Jumanne ijayo. Hata hivyo, taarifa ya nahodha huyo iliyotolewa na United imedai kuwa hana mpango wowote wa kuondoka Old Trafford msimu huu. Rooney amesema pamoja na kuwindwa na klabu zingine jambo ambalo anashukuru, ameamua kumaliza uvumi huo na kuongeza kuwa ataendelea kubakia United.

No comments:

Post a Comment