Friday, April 21, 2017

BEKI WA ZAMANI WA UINGEREZA AFARIKI.

BEKI wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Aston Villa, Ugo Ehiogu amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 44 baada ya kupata matatizo ya mshituko ya moyo wakati akiwa eneo la mazoezi la klabu ya Tottenham Hotspurs. Katika taarifa yake, Spurs wamedai kuwa Ehiogu alifariki dunia akiwa hospitali mapema leo. Ehiogu ambaye alikuwa kocha wa kikosi cha vijana chini ya umri wa miaka 23 cha Spurs, aliichezea Uingereza mechi nne. Ehiogu aliwahi kuichezea Villa zaidi ya mechi 200 kati ya mwaka 1991 na 200 na baadae kuja kuitumikia Middlesbrough kwa miaka saba.

No comments:

Post a Comment