Friday, April 21, 2017

MMOJA ASHITAKIWA KWA MILIPUKO BASI LA DORTMUND.

POLISI nchini Ujerumani wamemshitaki mtu mmoja kwa kuhusika na shambulio katika basi la timu ya Borussia Dortmund. Waendesha mashitaka wamedai kuwa mtu huyo ambaye ni mfanyabishara alifanya tukio hilo kwa lengo la kujipatia fedha kama bei za hisa ya timu hiyo zingeshuka. Mtu aliyejulikana kwa jina la Sergej W, mwenye umri wa miaka 18 alikuwa amteja katika hoteli ambayo timu hiyo ilifikia ambapo chumba chake kilikuwa kinetizamana na mtaa ambao milipuko ilitokea. Watu wawili walihitaji msaada wa kimatibabu baada ya mabomu matatu kulipuka karibu na basi la timu hiyo. Beki wa kimataifa wa Hispania, Marc Barta aliumia kiganja cha mkono na kufanyiwa upasuaji na afisa mmoja wa polisi naye alitibiwa kufuatia kupata mshituko.

No comments:

Post a Comment