Wednesday, April 26, 2017

MOURINHO KUENDELEA KUWAPA "MAKAVU LIVE" WACHEZAJI WAKE.

MENEJA wa Manchester United, Jose Mourinho amesisitiza kuwa hajali kama wachezaji wa kikosi chake hawapendi kukosolewa hadharani na kuongeza anadhani msimu huu unaweza kuwa wa kwanza wa miaka ya furaha Old Trafford. Henrikh Mkhitaryan, Luke Shaw, Anthony Martial na Chris Smalling wote wamewahi kukosolewa na Mourinho hadharani msimu huu. Lakini meneja huyo amesisitiza kuwa mbinu yake hiyo ni kwa ajili ya timu na kuwataka wachezaji ambao wanaonekana kushuka viwango vya kwa mara nyingine kufuata mfano unaoonyeshwa na Marcus Rashford. Akizungumza na Sky Sports kuhusiana na suala hilo, Mourinho amesema yeye hajali kwani anajaribu kuwa yeye kwa kuongeza kile anachoona sio sahihi. Mourinho aliendelea kudai kuwa kama mchezaji anacheza kwa kiwango chake bora hakuna cha ziada atakachoomba kutoka kwake.

No comments:

Post a Comment