Thursday, April 27, 2017

SHABIKI WA SPURS APIGWA NA MASHABIKI WENZAKE.

SHABIKI mmoja wa Tottenham Hotspurs alijikuta matatani na kuumizwa vibaya baada ya kushambuliwa na mashabiki wenzake wa timu hiyo ambayo walidhani ni shabiki wa Chelsea. Shabiki huyo, Michael Voller alikuta katika mkasa huo kufuatia mchezo wa nusu fainali kati ya klabu hizo mbili kutoka jiji la London uliofanyika katika Uwanja wa Wembley Jumamosi iliyopita. Tukio hilo linadaiwa kutokea nje ya mgahawa wa Moore Spice ambapo shabiki huyo alionekana na mashabiki wa Spurs akienda upande tofauti ndipo sakata hilo lilipomkuta. Voller alipigwa na kuumizwa vibaya kwa kuvunjwa taya pamoja na kuvimba uso kwa kipigo hicho.

No comments:

Post a Comment