Wednesday, May 24, 2017

CHELSEA YAAHIRISHA SHEREHE ZA UBINGWA.

KLABU ya Chelsea imeahirisha maandamano ya kusheherekea ubingwa wao wa Ligi Kuu Jumapili hii kufuatia shambulio la kigaidi jijini Manchester ambapo watu 22 walipoteza maisha. Mlipuaji wa kujitoa muhanga alilipua bomu katika tamasha la muziki lilifanyika Manchester Arena juzi ambapo watu zaidi ya 59 walijeruhiwa. Chelsea ambao wanatarajiwa kukwaana na Arsenal katika fainali ya Kombe la FA Jumamosi hii, walitoa taarifa leo kuthibitisha mpango wao wa kuhahirisha maandamano ya kusherekea taji lao. Katika taarifa yao, Chelsea wamedai kuwa wanaungana na watu wote ambao kwa namna moja au nyingine wameguswa na tukio hilo katika kuomboleza hivyo wanadhani haitakuwa vyema kuendelea na mipango yao ya sherehe kipindi hiki. Arsenal nao wamethibitisha kuahirisha onyesho la moja kwa moja la mchezo huo kutoka Wembley, ambalo lilipangw akufanyika kwenye Uwanja wa Emirates, na kuongeza hakutakuwa na maandamano ya sherehe kama wakishinda taji hilo.

No comments:

Post a Comment