Wednesday, May 31, 2017

LAUREN AUNGA MKONO WENGER KUONGEZWA MKATABA.

BEKI wa zamani wa kimataifa wa Cameroon na klabu ya Arsenal, Lauren anaamini kubaki kwa Arsene Wenger ni jambo zuri kwa timu hiyo. Meneja huyo ambaye alikuwa akikosolewa vikali msimu uliopita anatarajiwa kusaini mkataba mpya wa miaka miwili wakati wowote baada ya bodi kuafiki kumuongeza muda kocha huyo. Laureni aliyekuwa akicheza nafasi ya beki wa kulia katika kikosi cha Wenger kilichotwaa taji la Ligi Kuu msimu wa 2003-2004 bila kufungwa, anadhani ni jambo lenye tija kumbakisha kocha huyo. Lauren aliendelea kudai kuwa kikubwa anachotakiwa kufanya Wenger hivi sasa ni kuingia sokoni na kufanya usajili wa nguvu huku akihakikisha anawabakisha nyota wake akiwemo Alexis Sanchez na Mesut ozil.

No comments:

Post a Comment