Wednesday, May 31, 2017

CECH ATWAA TUZO NYINGINE NCHINI KWAO.

KIPA wa Arsenal, Petr Cech ametunukiwa tuzo ya Mpira wa Dhahabu ya kuwa mchezaji bora wa msimu wa 2016-2017 wa Jamhuri ya Czech. Hii ni mara ya 11 kwa golikipa huyo namba moja wa Arsenal kutwaa tuzo hiyo. Cech ameisaidia Arsenal kumaliza katika nafasi ya tano msimu huu na pia kutwaa taji la Kombe la FA kwa kuwafunga mabingwa Chelsea Jumamosi iliyopita. Tuzo hizo hutolewa kwa wanahabari wa michezo nchi humo kupiga kura na kuchagua wanasoka waliofanya vyema katika msimu husika.

No comments:

Post a Comment