Tuesday, May 30, 2017

MONACO YACHEMKA KA MAHREZ, ARSENAL NJIA NYEUPE.

KLABU ya Monaco inadaiwa kushindwa kinyang’anyiro cha kumsajili kiungo wa Leicester City, Riyad Mahrez na kuwaacha Arsenal wakipewa nafasi kubwa ya kumnasa. Mchezaji huyo bora Ligi Kuu msimu uliopita anafurahia kuishi Uingereza ambapo amekuwa mmoja kati ya mawinga bora duniani pamoja na kupoteza kiwango chake mwanzoni mwa msimu wa 2016-2017. Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger alizungumza kwa simu na Mahrez mwaka jana ambapo alimuelezea nia yake ya kumsajili ingawa dili hilo halikufanikiwa. Leicester sasa wanaonekana kuwa tayari kumuachia winga huyo kama watapata ofa stahiki ya uhamisho wake. Leicester waliomaliza nafasi ya 12 katika msimamo wa Ligi Kuu msimu huu wana matumaini ya kupata kiasi cha paundi milioni 35 kwa kiungo huyo.

No comments:

Post a Comment