Tuesday, May 30, 2017

DORTMUND YAMTIMUA TUCHEL.

KLABU ya Borussia Dortmund imemtimua meneja wake Thomas Tuchel kufuatia taarifa za mgawanyiko katika vyumba vya kubadilishia nguo na kumaliza kwenye nafasi ya tatu katika msimamo wa Bundesliga. Klabu ilithibitisha kuondoka kwake kufuatia kuzagaa kwa madai kuwa uhusiano wa Tuchel na wachezaji wa Dortmund ulikuwa umevurugika kiasi ambacho hakiwezi kusawazishwa. Ingawa Dortmund walishinda taji la DFB Pokal Jumamosi iliyopita, lakini bado ilionekana uhusiano baina yake na wachezaji hautaweza kutengemaa. Nahodha wa klabu hiyo Marcel Schmelzer na mshambuliaji mwenye ushawishi Marco Reus wote walijiweka pembeni na kocha huyo mwenye umri wa miaka 43 ambaye atapokea kiasi cha euro milioni 2.9 kama kiinua mgongo chake. Tuchel alichukua nafasi ya Jurgen Klopp mwaka 2015 wakati kocha huyo alipondoka Signal Iduna Park baada ya Dortmund kumaliza msimu wakiwa nafasi ya saba.

No comments:

Post a Comment