Tuesday, May 30, 2017

WENGER AKUBALI MIAKA MIWILI ZAIDI ARSENAL.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amekubali kusaini mkataba mpya wa miaka miwili wa kuendelea kuinoa klabu hiyo aliyoiongoza kwa miaka 21. Wenger na mmiliki wa klabu Stan Kroenke walikutana jana ili kujadiliana mustakabali wake, huku uamuzi ukipelekwa kwa wakurugenzi kwenye kikao cha bodi kilichofanyika hii leo. Arsenal inapanga kutoa taarifa rasmi kuhusiana na suala hilo kesho. Klabu hiyo ilimaliza katika nafasi ya tano katika msimamo wa Ligi Kuu msimu huu, ikiwa ni mara ya kwanza kumaliza nje ya nne bora toka meneja huyo raia wa Ufaransa alipojiunga nao mwaka 1996. Arsenal walimaliza wakiwa alama 18 nyuma ya mabingwa Chelsea, lakini waliwachapa mabingwa hao kwa mabao 2-1 na kutwaa Kombe la FA katika Uwanja wa Wembley Jumamosi iliyopita.

No comments:

Post a Comment