Tuesday, May 30, 2017

AC MILAN YANASA BEKI WA VILLARREAL.


KLABU ya AC Milan imetangaza kumsajili beki wa kati Mateo Musacchio kutoka Villarreal kwa mkataba wa miaka minne. Beki huyo alifanyiwa vipimo vya afya wiki iliyopita na sasa ameshakamilisha uhamisho wake San Siro huku ikiaminika kuwa Milan wamelipa kiasi cha euro milioni 18. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26, alianza soka lake katika klabu ya River Plate kabla ya kujiunga na Villarreal mwaka 2009. Akiwa Villarreal Musacchio amefanikiwa kucheza zaidi ya mechi 200 za mashindano yote lakini sasa atatua Serie A. Milan walimaliza katika nafasi ya sita kwenye Serie A msimu wa 2016-2017 na kufuzu michuano ya Europa League, lakini wanataka wamepanga msimu ujao kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment