Tuesday, May 30, 2017

SOUTHGATE AELEZA SABABU ZA KUMUACHA ROONEY.

KOCHA wa timu ya taifa ya Uingereza, Gareth Southgate amesema hakuzungumza na nahodha Wayne Rooney kabla ya kufikia uamuzi wa kumuacha katika kikosi chake kwa ajili ya mechi za mwezi ujao dhidi ya Scotland na Ufaransa. Rooney ambaye ndio mfungaji bora wa wakati wote Uingereza ameanza katika mechi 15 pekee za ligi akiwa na Manchester United msimu huu. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 31, aliachwa pia katika kikosi kilichoitwa Machi mwaka huu kutokana na majeruhi. Akizungumza na wanahabari, Southgate amesema sababu kubwa iliyomfanya kumuacha Rooney kipindi hiki ni kiwango bora kilichoonyeshwa na wachezaji wengine wan chi hiyo.

No comments:

Post a Comment