Tuesday, May 30, 2017

MWENYEKITI WA CITY ADAI AGUERO HAENDI KOKOTE.

MWENYEKITI wa Manchester City, Khaldoon Al Mubarak amesema mustakabali wa Sergio Aguero hauna mashaka yeyote. Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 28, ana mkataba na klabu hiyo unaomalizika mwaka 2020 lakini alipoteza nafasi yake kwenye kikosi cha kwanza Februari mwaka huu mbele ya chipukizi mwenye umri wa miaka 19 Gabriel Jesus. Aguero ambaye alijiunga na City akitokea Atletico Madrid kwa kitita cha paundi milioni 38 mwaka 2011, alikaririwa Machi mwaka huu akidai kuwa hataki kuondoka katika klabu hiyo. Akiulizwa kuhusu mustakabali wa nyota huyo, Al Mubarak amesema ni mmoja kati ya wachezaji bora duniani hivyo lazima abakie.

No comments:

Post a Comment