Saturday, May 27, 2017

MAN CITY YAMMENDEA KIPA WA BENFICA.

KLABU ya Manchester City inaweza kumfanya kipa wa Benfica, Ederson kuwa kipa ghali zaidi katika historia ifikapo wiki ijayo. Taarifa kutoka nchini Ureno zinadai kuwa City wana uhakika wa kukamilisha taratibu za kumsajili kipa huyo mara baada ya kumalizika kwa fainali ya Kombe la Ureno kesho ambapo Benfica watacheza na Vitoria Guimaraes. City wanaweza kulazimika kulipa kiasi cha paundi milioni 35 kwa ajili ya kipa huyo mwenye umri wa miaka 35, kiasi ambacho kitapita kile cha paundi milioni 33 Juventus walizotoa kwa Parma kwa ajili ya kusajili Gianluigi Buffon mwaka 2001. Benfica wanamilika asilimia 50 pekee za haki ya Ederson hivyo watahitaji kiasi kikubwa cha ada ya usajili kwani watalazimika kugawana nusu kwa nusu na klabu yake ya zamani ya Brazil ya Rio Ave na wakala wa soka wa Gestifute. Jorge Mendes ambaye alikuwa jijini Manchester kusimamia uhamisho wa Bernardo Silva kwenda City ndiye wakala wa Ederson na mmiliki wa kampuni ya Gestifutre.

No comments:

Post a Comment