Saturday, May 27, 2017

BARCELONA YAPATA AHUENI.

KLABU ya Barcelona imepata ahueni katika safu yao ya ulinzi kuelekea katika mchezo wao wa fainali ya Kombe la Mfalme baadae leo kufuatia taarifa za kuwepo kwa Gerard Pique, Javier Mascherano na Aleix Vidal. Pique alikosa mechi mbili za mwisho za La Liga za Barcelona kutokana na maumivu ya tumbo wakati Mascherano yeye alikosa mchezo walioshinda 4-2 dhidi ya Eibar kutokana na majeruhi ya msuli wa paja. Kurejea kwa Vidal ni jambo la kushangaza kidogo kwa hapo awali beki huyo wa kulia ilielezwa kuwa atakosa msimu wote uliosalia baada ya kupata majeruhi ya kifundo cha mguu katika mchezo walioshinda mabao 6-0 dhidi ya Alaves Februari mwaka huu. Mshambuliaji Luis Suarez na beki Sergi Roberto watakosa mchezo huo kutokana na kutumikia adhabu wakati Jeremy Mathieu na Rafinha wao wakiwa nje bado kwa majeruhi. Barcelona watakuwa wakifukuzia rekodi ya kutwaa taji hilo kwa mara ya 29 wakati watakapoivaa Alaves baadae leo huku pia ukiwa mchezo wa mwisho wa meneja Luis Enrique.

No comments:

Post a Comment