Saturday, May 27, 2017

WATFORD WAPATA KOCHA MPYA.

KLABU ya Watford imemteua meneja wa zamani wa Hull City, Marco Silva kuwa meneja wao mpya kwa mkataba wa miaka miwili. Silva anakuwa meneja wa tisa wa Watford katika kipindi cha miaka mitano na nane toka familia ya Pozzo ya Italia ilipochukua umiliki wa timu hiyo mwaka 2012. Meneja huyo raia wa Ureno mwenye umri wa miaka 39 alichukua mikoba ya Mike Phelan Hull City Januari mwaka huu lakini alishindwa kuiwezesha kutoshuka daraja msimu huu na kujizulu Alhamisi iliyopita. Mwenyekiti wa Watford, Scott Duxbury amesema Silva ni mmoja kati ya makocha wazuri kwasasa kwenye Ligi Kuu na imani yao atawasaidia kwa ajili ya msimu ujao.

No comments:

Post a Comment