Friday, May 26, 2017

MAN CITY YANASA KIUNGO WA MONACO.

KLABU ya Manchester City imekubali kutoa kitita cha paundi milioni 43 kwa ajili ya kumsajili kiungo wa kushambulia Bernardo Silva kutoka kwa mabingwa wa Ufaransa Monaco. Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno mwenye umri wa miaka 22, anatarajiwa kujiunga na City pindi dirisha la usajili la majira ya kiangazi likapofunguliwa Julai mosi mwaka huu huku klabu ikitarajiw akutangza usjaili huo Alhamisi ijayo. Silva amecheza mechi 58 akiwa na Monaco msimu huu zikiwemo mechi mbili dhidi ya City walizokutana katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, ambapo amefunga mabao 11 na kusaidia mengine 12. Nyota huyo pia ameichezea Ureno mara 12 na kufunga bao moja.

No comments:

Post a Comment