Wednesday, May 24, 2017

SCHALKE ILIMWANIA PULISIC.

MKURUGENZI wa Schalke 04, Oliver Ruhert amebainisha klabu hiyo ilitaka kumsajili Christian Pulisic kabla ya hajaimarika kimataifa kwa mahasimu wao Borussia Dortmund. Pulisic amewateka mashabiki wa Dortmund toka alipohamia hapo akitokea Marekani na kupelekea kujihakikishia nafasi katika kikosi cha kwanza cha meneja Thomas Tuchel msimu huu. Pulisic mwenye umri wa miaka 18 amefunga mabao matano katika mechi 42 alizocheza katika mashindano yote na kuiwezesha timu hiyo kushika nafasi ya tatu katika msimamo wa Bundesliga. Hata hivyo, angeweza kugeuka adui wa timu yake ya sasa wakati Schalke walipomuwania lakini walichelewa kwani mustakabali wake tayari ulishaamuliwa. Ruhert amesema tayari walikuwa wameshaanza mazungumzo na wakala wake kuhusu kumsajili lakini waliambiwa kuwa tayari walikuwa wameshakubali ofa ya Dortmund.

No comments:

Post a Comment