Wednesday, May 24, 2017

FIFA WAIPONGEZA YANGA KUTWAA UBINGWA.

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Gianni Infantino ametuma salama za pongezi kwa klabu ya Yanga kufuatia kutwaa taji la la Ligi Kuu Tanzania Bara kwa mara ya tatu mfululizo mwishoni mwa wiki iliyopita. Taarifa hizo za pongezi zimetolewa kupitia barua yake aliyotuma kwa Shirikisho la Soka nchini-TFF kwenda kwa Katibu Mkuu wa Yanga Boniface Mkwasa. Rais wa TFF, Jamal Malinzi alithibitisha taarifa hizo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter na kudai kuwa barua rasmi kutoka FIFA atakabidhiwa Mkwasa. Yanga walitawadhwa mabingwa kwa mara nyingine Jumamosi iliyopita kwa kuwazidi mahasimu wao Simba kwa tofauti ya mabao ya kufungwa na kufunga baada ya kulingana alama wote wakiwa na alama 68 katika michezo 30.

No comments:

Post a Comment