Wednesday, May 31, 2017

WOLFSBURG YAANZA USAJILI KWA KISHINDO.

BEKI wa kimataifa wa Marekani, John Brooks ameondoka Hertha Berlin na kusajiliwa na Wolfsburg kwa ada inayoripotiwa kuvunja rekodi kwa raia wa Marekani. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 amejiunga na Wolfsburg baada kupita misimu mitano akiwa hertha Berlin ambapo sasa amesaini mkataba unaomalizika mwaka 2022. Taarifa zinadai kuwa Wolfsburg imetoa kitita cha dola milioni 22.5 hivyo kuvunja rekodi iliyokuwepo ya dola milioni 13 wakati Jozy Altidore aliposajiliwa na Sunderland akitokea AZ mwaka 2013. Brooks ambaye ametokana na matunda ya akademi ya Hertha, ameichezea klabu hiyo mechi 24 na kuisaidia kumaliza katika nafasi ya sita kwenye Bundesliga msimu wa 2016-2017.

No comments:

Post a Comment