Wednesday, May 31, 2017

IBRAHIMOVIC KUBAKI LIGI KUU.

WAKALA wa Zlatan Ibrahimovic amedai kuwa mteja wake huyo anataka kubakia katika Ligi Kuu ya Uingereza lakini sio lazima kwamba atabakia Manchester United. Mshambuliaji huyo wa zamani wa kimataifa wa Sweden, anakabiliwa na majeruhi ya muda mrefu baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti na mkataba wake na United unatarajiwa kumalizika mwezi ujao. Meneja wa United Jose Mourinho alishadokeza kuwa anataka mshambuliaji huyo abakie Old Trafford, lakini majeruhi yake yanafanya mambo kuwa magumu. Hata hivyo, Wakala wake Mino Raiola amesema kuna uwezekano wa Ibrahimovic kubakia Old Trafford lakini pia anaweza kuondoka kwani wameshapata ofa kadhaa.

No comments:

Post a Comment