Wednesday, May 31, 2017

DE ROSSI APEWA MKATABA MWINGINE ROMA.

MSHAMBULIAJI Daniele De Rossi amesaini mkataba mpya na AS Roma ambao utamuweka katika klabu hiyo mpak Juni mwaka 2019. Roma ilimuaga nguli wake Francesco Totti mwishoni mwa wiki iliyopita, lakini sasa wamefanikiwa kumbakisha nyota mwingine. Mkataba wa De Rossi ulikuwa unamalizika mwezi ujao lakini sasa amesaini mwingine wa miaka miwili zaidi. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 33 aliibuliwa kutoka katika akademi ya klabu na amefanikiwa kucheza jumla ya mechi 561 katika mashindano yote toka aibukie katika kikosi cha kwanza mwaka 2001 na kufunga mabao 59. De Rossi amekuwa mchezaji muhimu msimu huu ambapo Roma imemalizika katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Serie A na kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.

No comments:

Post a Comment