Wednesday, May 31, 2017

GRIEZMANN AMTUPIA MZIGO RAIS WA ATLETICO.

MSHAMBULIAJI wa Atletico Madrid, Antoine Griezmann amesema anafurahia kuwepo klabu hapo na kuwa mustakabali wake uko mikononi mwa rais wa timu hiyo. Akizungumza na wanahabari, Griezmann amedai anajisikia furaha kuwepo hapo na wakala wake anazungumza na Atletico hivyo wataona kitakachotokea. Griezmann aliendelea kudai kuwa atafanya uamuzi wake majira haya ya kiangazi. Nyota huyo ambaye anahusishwa na tetesi za kwenda Manchester United, amesema tayari ameshazungumza na kocha na sasa suala lake liko mikononi mwa rais wa klabu.

No comments:

Post a Comment