Monday, June 26, 2017

MOURINHO AFIWA NA BABA YAKE.

BABA yake meneja wa Manchester United, Jose Mourinho aitwaye Felix Mourinho amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 79. Taarifa za kifo cha mzee huyo zimethibitishwa na klabu yake ya zamani ya Belenenses. Felix aliichezea klabu hiyo kwa kipindi kirefu akiwa kama kipa na baadae kupata nafasi ya kuichezea Ureno mara moja kabla ya kustaafu na kuanza kutafuta vipaji kazi ambayo ndio ilipelekea mwanae Jose kuja kujulikana na kuwa kocha bora duniani. Kufuatia kifo hicho Mourinho alituma picha akiwa na baba yake katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram bila kuweka ujumbe wowote. Mazishi ya Felix yanatarajiwa kufanyika huko Setubal kesho.

No comments:

Post a Comment