Tuesday, July 25, 2017

BARCELONA YAITIA LIVERPOOL TUMBO JOTO KWA COUTINHO.

KLABU ya Barcelona imegoma kuacha mbio zake za kumuwania kiungo wa Liverpool Philippe Coutinho kufuatia maafisa wake kudaiwa kusafiri kuelekea jijini London kujaribu kufanikisha uhamisho huo. Taarifa kutoka nchini Hispania zinadai kuwa Barcelona inaamini dili hilo linaweza kufanikiwa kwa kutoa kitita cha paundi milioni 90. Meneja wa Liverpool amesisitiza Coutinho mwenye umri wa miaka 25 bado ataendelea kuwepo katika mipango yake kwa ajili ya msimu ujao na hana mpango wowote wa kumuachia nyota huyo wa kimataifa wa Brazil. Akizungumza na wanahabari mwishoni mwa wiki iliyopita, Klopp amesema kila mtu anafahamu kuwa Coutinho ni mchezaji muhimu kwao na mwenyewe anafahamu kuwa anajisikia vyema wakati wote anapokuwa katika klabu hiyo. Taarifa kutoka Hispania zimedai kuwa maafisa wa Barcelona walikutana na wawakilishi wa Liverpool na mawakala wanaofanya kazi kwa niaba ya Coutinho katika safari hiyo ya Uingereza. Coutinho alijiunga na Liverpool akitokea Espanyol kwa kitita cha paundi milioni 8.5 Januari mwaka 2013.

No comments:

Post a Comment