Tuesday, July 25, 2017

MBAPPE ANUKIA MADRID KWA ADA YA KUFURU.

TAARIFA kutoka nchini Hispania zimedai kuwa Real Madrid hatimaye wamefikia makubaliano na Monaco kwa ajili ya mshambuliaji Kylian Mbappe. Madrid wanadaiwa kukubali kutoa kitita cha paundi milioni 161 ka ajili ya chipukizi huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 18. Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa na gazeti la Marca, Madrid wamekubali kulipa paundi milioni 145 kama ada ya awali kwa mchezaji huyo huku nyingine paundi milioni 16 wakija kuilipa baadae. Madrid wanataka kumnasa chipukizi huyo kufuatia kumuacha Alvaro Morata kwenda kujiunga na Chelsea. Monaco walikuwa wakitaka kumbakisha Mbappe katika klabu hiyo kipindi hiki cha kiangazi lakini ofa hiyo mpya ya Madrid ambayo itavunja rekodi ya dunia inaweza kuwashawishi kumuachia.

No comments:

Post a Comment