Tuesday, July 25, 2017

RONALDO AMALIZA UVUMI WA KUONDOKA MADRID.

TETESI za mustakabali wa Cristiano Ronaldo sasa zimefikia tamati kufuatia nyota huyo kuliambia gazeti moja nchini Hispania kuwa atabakia Real Madrid kwa ajili ya kushinda mataji zaidi. Akikaririwa na gazeti la Marca katika mahojiano huko Shanghai, Ronaldo amesema kushinda mataji muhimu na klabu na kwake binafsi msimu uliopita lilikuwa jambo zuri hivyo kufanya hivyo tena itakuwa fahari. Kufuatia kauli yake hiyo ni wazi kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Ureno anataka kubakia Santiago Bernabeu kwa msimu ujao pamoja na tetesi zilizozagaa kuhusu mustakabali wake kwa miezi kadhaa. Jumamosi iliyopita meneja wa Madrid Zinedine Zidane aliwahakikishia mashabiki wa klabu hiyo kuwa Ronaldo kwasasa yuko likizo na atarejea katika kikosi hicho Agosti 5 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment