Tuesday, July 25, 2017

CHICHARITO NDANI YA WEST HAM.

KLABU ya West Ham United imefnikiwa kukamilisha usajili wa paundi milioni 16 wa mshambuliaji Javier Hernadez kutoka bayer Leverkusen ya Ujerumani. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester United amepewa mkataba wa miaka mitatu na klabu hiyo ya Ligi Kuu. Mei mwaka huu Hernandez ambaye anajulikana zaidi kwa jina la utani la Chicharito, alifanikiwa kuwa mfungaji bora wa wakati wa kikosi cha timu ya taifa ya Mexico. Akizungumza na wanabahari, Hernandez amesema Ligi Kuu ya Uingereza ndio bora duniani na pindi nafasi ilipopatikana alifurahia sana kujiunga na klabu hiyo. Hernandez mwenye umri wa miaka 29, amefunga mabao 59 katika mechi 156 alizochezea United baada ya kutua Old Trafford mwaka 2010 kabla ya kujiunga na Leverkusen kwa kitita cha paundi milioni 7.3 Agosti mwaka 2015. Akiwa Leverkusen, Hernandez amefanikiwa kufunga mabao 39 katika mechi 76 alizoichezea klabu hiyo ya Bundesliga.

No comments:

Post a Comment