Tuesday, July 25, 2017

CHALSEA YAMRUDISHA NYUMBANI NYOTA WAKE KWA KAULI YA KIBAGUZI, WAPIGWA TATU NA BAYERN.

KLABU ya Chelsea imemrudisha nyumbani Kenedy kutoka katika ziara yao ya maandalizi ya msimu mpya kufuatia kauli aliyotoa nyota huyo katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii kabla ya mchezo wao huko China. Klabu hiyo iliomba radhi baada ya mashabiki kumtuhumu nyota huyo mwenye umri wa miaka 21 kwa ubaguzi na chuki dhidi ya wageni. Kenedy aliweka ujumbe huo kwenye ukurasa wake wa Instagram kabla ya mchezo walioshinda mabao 3-0 dhidi ya Arsenal, ambapo mashabiki walikuwa wakimzomea wakati wa mchezo. Kenedy baadae aliomba radhi lakini Chelsea waliamua kuchukua hatua zaidi kwa kumrejesha nyumbani na kumuondoa katika ziara yao. Mapema leo Chelsea ilitandikwa mabao 3-2 katika mchezo wao mwingine wa kirafiki dhidi ya Bayern Munich uliochezwa kwenye Uwanja wa taifa nchini Singapore.

No comments:

Post a Comment