Tuesday, July 25, 2017

WOLVES YANASA CHIPUKIZI KUTOKA ATLETICO.

KLABU ya Wolves imefanikiwa kumsajili chipukizi wa kimataifa wa Ureno Diogo Jota kwa mkopo wa msimu mzima kutoka Atletico Madrid. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 20 alicheza kwa mkopo katika klabu ya FC Porto ambapo alicheza chini ya meneja Nuno Espirito Santo anayeinoa Wolves kwasasa. Jota alianza soka lake katika klabu ya nyumbani ya Pacos Ferreira na baadae kujiunga na Atletico kwa mkataba wa miaka mitano kiangazi mwaka jana. Akizungumza na wanahabari, Jota amesema hiyo nafasi nzuri wake kujiimarisha chini ya meneja ambaye anamuamini. Jota alifunga mabao tisa katika mechi 35 alizoichezea Porto msimu uliopita, likiwemo bao moja alilofunga katika ushindi wa mabao 5-0 waliopata kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Leicester City Desemba mwaka jana.

No comments:

Post a Comment