Monday, July 24, 2017

MORATTA APEWA NAMBA 9 CHELSEA.

KLABU ya Chelsea, imethibitisha kuwa nyota mpya Alvaro Morata aliyesajiliwa hivi karibuni atakuwa anavaa jezi yenye namba 9 katika msimu wa 2017-2018. Chelsea ilikamilisha usajili wa mshambuliaji huyo kutoka Real Madrid kwa kitita cha paundi milioni 70 Julai 21 mwaka huu na kumpa mkataba wa miaka mitano. Na sasa klabu hiyo imebainisha kuwa Morata atakuwa akivaa jezi namba 9 ambayo haikuwa ikivaliwa na mchezaji yeyote msimu uliopita. Mchezaji wa mwisho kuvaa jezi yenye namba hiyo alikuwa Radamel Falcao ambaye aliivaa msimu wa 2015-2016.

No comments:

Post a Comment