Monday, July 24, 2017

ANCELOTTI AKOMAA NA ARTURO VIDAL.

MENEJA wa Bayern Munich, Carlo Ancelotti amedai kuwa hakuna uwezekano wa Arturo Vidal kuondoka katika klabu hiyo lakini amekiri kuwa Renato Sanchez anaweza kuondoka. Kuna tetesi kuwa United ilikuwa ikiwawania viungo hao lakini Ancelotti amekanusha kuwa Vidal hatakwenda popote kipindi hiki cha majira ya kiangazi. Akizungumza na wanahabari kuhusiana na suala hilo, Ancelotti amesema hakuna uwezekano huo kwani Vidal ni mchezaji wao na ana uhakika na hilo. Kuhusu suala la Sanchez Ancelotti alikiri kuwa kuna uwezekano nyota huyo akabaki au akaondoka lakini kwa hivi sasa bado wako naye na anafanya mazoezi

No comments:

Post a Comment