Monday, July 24, 2017

CONTE ATOA HOFU HALI YA PEDRO.

MENEJA wa Chelsea, Antonio Conte amesema Pedro alipata majeraha kadhaa kufuatia kugongana na kipa wa Arsenal David Ospina kwenye mchezo wa kirafiki uliofanyika Jumamosi iliyopita lakini anatarajiwa kurejea mazoezi ndani ya siku 10 zihazo. Winga huyo mwenye umri wa miaka 29 alikimbizwa hospitalia kufuatia mchezo huo uliofanyika jijini Beijing, ambapo Chelsea walishinda mabao 3-0 na kulazwa kwa siku moja. Pedro pia alipata mtikisiko wa ubongo lakini alituma ujumbe akidai kuwa kila kitu kiko sawa kabla ya kusafiri kurejea jijini London. Pedro anatarajiwa kuvaa kitu cha kukinga uso wake wakati atakaporejea mazoezini. Kikosi cha Chelsea kilichosalia kwasasa kiko Singapore ambapo watacheza mechi mbili dhidi ya Bayern Munich kesho na Inter Milan Julai 29

No comments:

Post a Comment