Monday, July 24, 2017

MENDY RASMI MAN CITY.

BEKI wa Monaco Benjamin Mendy amekamilisha usajili wake wa paundi milioni 52 kwenda Manchester City. Beki huyo wa kushoto wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 23, ambaye alijiunga na Monaco akitokea Marseille kiangazi mwaka jana, amesaini mkataba wa miaka mitano na klabu hiyo. Mendy anakuwa mchezaji wa tano kusajiliwa na City kipindi hiki cha usajili wa kiangazi na kupelekea klabu hiyo kutumia zaidi ya paundi milioni 200. Mendy ameichezea mechi 34 Monaco msimu uliopita na kuisaidia kushinda taji lao la kwanza la Ligue 1 baada ya kupita miaka 17. Mbali na Mendy nyota wengine waliosajiliwa na City mpaka sasa ni pamoja na nyota wa kimataifa wa Kyle Walker paundi milioni 45, kiungo wa kimataifa wa Ureno Bernardo Silva paundi milioni 43, kipa wa kimataifa wa Brazil Ederson Moraes paundi milioni 35 na kiungo Danilo kutoka Real Madrid paundi milioni 26.5.

No comments:

Post a Comment