Monday, July 24, 2017

VAN DIJK AACHWA KIKOSI CHA SOUTHAMPTON.

NAHODHA wa Southampton Virgil van Dijk ameondolewa katika kikosi cha timu hiyo ambacho kitakwenda kuweka kambi mazoezi nchini Ufaransa wiki hii. Beki huyo mwneye umri wa miaka 26, amekuwa akihusishwa na tetesi za kwenda Liverpool, ingawa klabu hiyo ya Anfield ilidai mwezi uliopita kuwa wameshaacha kumfuatilia. Southampton tayari ilishaweka wazi kuwa hawana mpango wowote wa kumuuza nyota huyo wa kimataifa wa Uholanzi. Wiki iliyopita meneja wa Southampton Mauricio Pellegrino amesema kuwa Van Dijk amekuwa akifanya mazoezi mwenyewe kwasababu anadhani mchezaji huyo hayuko sawa kwa asilimia 100. Van Dijk ambaye alijiunga na Southampton mwaka 2015 akitokea Celtic, alisafiri na kikosi cha timu hiyo kilichofanya ziara ya maandalizi ya msimu mpya huko Austria mapema mwezi huu lakini Pellegrino ameamua kumuacha kwenye safari yao ya Ufaransa.

No comments:

Post a Comment