Thursday, July 20, 2017

MAJERUHI YAMKOSESHA THIAGO ALCANTARA PRE-SEASON.

KIUNGO Thiago Alcantara anatarajiwa kukosa mechi kadhaa za Bayern Munich kujiandaa na msimu mpya dhidi ya AC Milan, Chelsea na Inter Milan kutokana na majeruhi ya misuli. Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania hakuwepo katika kikosi cha Bayern kilichocheza mechi ya Kombe la Ubingwa wa Kimataifa dhidi ya Arsenal iliyofanyika huko Shanghai jana na anatarajiwa kurejea nchini Ujerumani kwa matibabu. Thiago alianza katika mechi 26 msimu uliopita akiwa na Bayern na kuisaidia kutwaa taji la tano mfululizo la Bundesliga ikiwa ni msimu wake mzuri kati ya minne aliyochezea timu hiyo. Meneja wa Bayern, Carlo Ancelotti amesema kwa pamoja yeye, madaktari na mchezaji wameamua ataendelea na kufanya mazoezi binafsi nyumbani wakati akijiuguza majeruhi yake hayo. Bayern wanatarajiwa kurejea katika mechi za ushindano Agosti 5 wakati watakapovaana na Borussia Dortmund katika mchezo wa DFL Supercup.

No comments:

Post a Comment