Thursday, July 20, 2017

WEST HAM YAKARIBIA KUMNASA CHICHARITO.

KLABU ya West Ham United inakaribia kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Mexico Javier Hernandez kutoka Bayer Leverkusen. Klabu hiyo ina uhakika wa kusamjili mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester United mwenye umri wa miaka 29, ingawa hakuna ada yeyote iliyowekwa wazi. Kwa upande mwingine, mshambuliaji wa Austria Marko Arnautovic anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya katika muda wa saa 48 zijazo baada ya West Ham kufikia makubaliano na Stoke City. Ofa mbili za West Ham zilikataliwa lakini inaaminika kuwa sasa Stoke wamekubali kupokea ada inayokadiriwa kufikia paundi milioni 24.

No comments:

Post a Comment