Thursday, July 20, 2017

MILAN YATHIBITISHA KUMNASA BONUCCI.

KLABU ya AC Milan imethibitisha rasmi kumnasa beki Leonardo Bounucci kutoka Juventus ya Italia. Milan imemnasa nyota huyo wa kimataifa wa Italia kwa mkataba wa miaka na ada inayokadiriwa kufikia euro milioni 42. Milan ilithibitisha Ijumaa iliyopita kuwa wamefikia makubaliano ya kumsajili Bonucci mwenye umri wa miaka 30, wakisubiri vipimo vyake vya afya. Lakini sasa Milan chini ya meneja Vincenzo Montella amebainisha kuwa usajili huo umekamilika.  Meneja wa Milan, Montella amesema Bonucci ni mchezaji mwenye uzoefu wa kimataifa na kiufundi anadhani yeye pamoja na Sergio Ramos ndio mabeki bora wa kati duniani.

No comments:

Post a Comment