Thursday, July 20, 2017

JUVENTUS YANASA BEKI WA AC MILAN.

KLABU ya Juventus imefanikiwa kumnasa beki wa kimataifa wa Italia Mattia De Sciglio kwa kitita cha euro milioni 12 kutoka AC Milan. Beki huyo amesajiliwa kwa mkataba wa miaka mitano na mabingwa hao wa Serie A na hatakuwa sehemu ya mabadiliko ya Milan chini meneja wake Vincenzo Montella. Beki huyo wa kulia anategemewa kuchukua nafasi ya Dabi Alves, baada ya nyota huyo wa kimataifa wa Brazil kutimkia Paris Saint-Germain-PSG kufuatia kukaa msimu mmoja jijini Turin. Ujio wa De Sciglio umekuja siku moja baada ya Juventus kumsajili Wojciech Szczesny kutoka Arsenal na kuongeza idadi ya wachezaji waliosajili akiwemo Rodrigo Bentancur na Douglas Costa.

No comments:

Post a Comment