Friday, July 28, 2017

CHELSEA YATENGA PAUNDI MILIONI 50 KWA BARKLEY NA CHAMBERLAIN.

KLABU ya Chelsea inadaiwa kutenga kitita cha paundi milioni 50 kwa ajili ya kuwawania nyota wawili wa kimataifa wa Uingereza, Ross Barkley na Alex Oxlade-Chamberlain. Meneja wa Chelsea Antonio Conte anataka kuongeza idadi ya wachezaji wazawa kwenye kikosi chake kufuatia kwasasa kuwa na idadi ya wachezaji 17 wa kigeni kwenye kikosi cha wachezaji 25. Kwa kipindi kirefu Chelsea imekuwa ikimfuatilia Barkley anayekipiga Everton, huku kiungo huyo alibakisha mwaka mmoja kwenye mkataba wake akikataa kuongeza mwingine. Meneja wa Everton Ronald Koeman tayari ameshamwambia Barkley kutafuta timu nyingine huku akihitaji kiasi cha paundi milioni 25. Kwa upande wa Chamberlain mwenye umri wa miaka 23 yeye pia amebakisha miezi 12 kwenye mkataba wake huku akiwa bado kupewa ofa mpya.

No comments:

Post a Comment